![]() |
| OF JESUS CHRIST |
NEEMA YA BWANA YESU
UTANGULIZI
Kabla hatuajaenda ndani zaidi hebu fuatana nami kwa
kusoma mistari hii;
2koritho 13:14
“Neema
ya Bwana Yesu Kristo na upendo
wa Mungu na
ushirika wa Roho Mtakatifu ukae
nanyi
nyote”
Rumi 16:24 &
2Thesolonike 3:18
“Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe
nanyi nyote”.
Galatia 6:18, filipi
4:23& filemoni 1:25
“Ndugu zangu, neema
ya Bwana wetu
Yesu Kristo
ikae pamoja na roho zenu.”
Efeso 6:24
“Neema iwe na wote wampendao
Bwana wetu Yesu Kristo kwa pendo wa dhati”
Karibu kila mstari ambao Paulo alikuwa anawaandikia
kanisa wa mahali mbalimabali ulimwenguni alikuwa anahusanisha maneno “Neema ya
Yesu Kristo”
Je umewahi kujiulizaau kutafakari ni kwanini
·
Paulo alikuwa anarudia rudia haya maneno
karibu nyaraka zake nyingi.
·
Je hii ilikuwa ni sehemu ya maombi ya Paulo
akiwaombea watu wa kanisa?
·
Zilikuwa ni Baraka Paulo alikuwa
anawabariki watu wake?
·
Kwanini mara zote alikuwa anasema Neema
ya Bwana Yesu Kristo na asiseme Neema ya Mungu au Neema ya Roho Mtakatifu?
Katika nyaraka
tulizopitia hapo awali, Paulo alikuwa natafautisha vitu vitatu na nani mhusika
kwa kila kimoja. Tazama pale aliposema “Neema” alisema ni ya Yesu kristo,
aliposema “Pendo” aliunganisha na Mungu na aliposema juu ya” Ushirika” alimtaja
Roho Mtakatifu.
MUNGU NI PENDO
Hapo mwanzo Neno alipokuwa ndani ya Mungu , Mungu alimtoa
Neno toka ndani yake, naye Neno akachukua mwili na kuja kwetu akaja kwa jina la
Yesu (Yohana 1:1-4,14). Kile kitendo cha Mungu kumtoa Neno aje kwetu kilikuwa
ni cha upendo, alitupenda sisi kuliko hata mwanae ( Yohana 3:16) hakuona
thamani ya mwanae kuwa ni kitu kwake, bali thamani yangu mimi na wewe ndio
aliona ni kitu cha thamani kwake. Sasa
Mungu mwenyewe ni PENDO ndani ya huyu Pendo kumezaliwa karama yake ya Upendo.
Yesu hakuja kwetu duniani sababu alikuwa anatupenda,
bali alikuja duniani kwa sababu ya KUMTII Baba yake (Ebrania 3:2 na Filipi
2:8). Yesu alikuwa na Upendo kwa Baba yake hata akakubali kutii hata kufuka
kifo cha msalaba. Kifo cha msalaba hakikupngwa na Yesu bali na Mungu mwenyewe
kwani ndiye aliyekuwa na Penzi/Pendo kwa mwanadamu.
Tazama hata Yesu mwenyewe
alipokuwa anazungumza na wanafunzi wake, aliwaambia ” Kama vile Baba alivyonipenda Mimi, hivyo ndivyo Mimi nilivyowapenda ninyi. Basi kaeni
katika pendo Langu” kuwa yeye (Yesu)
hakuwa na upendo kwetu, ILA sababu na kwakuwa BABA yake alikuwa anampenda yeye
( mwanae) basin a yeye (Yesu) akajikuta/akawahana budi kutupenda sisi. Kwa
lugha rahisi ni kuwa Pendo la Yesu Kwetu limesababishwa na Mungu kwanza
kumpenda Yesu. Ila Pendo la Mungu kwetu halina sababu.
Hivyo Paulo anaposema juu ya Pendo anamaanaisha ni
Mungu tu ndiye awezaye kukupenda mwanadamu bila sababu au kuchochewa na
chochote. Na ni yeye peke yake mwenye
hiyo hali ya Kupenda.
ROHO MTAKATIFU NI MSHIRIKA.
Biblia katika mistari tuliyosoma hapo
awali, inasema juu ya ushirika kuwa u ndani ya Roho Mtakatifu.
Yohana 14:26
Lakini huyo Msaidizi, yaani, huyo Roho Mtakatifu,
ambaye
Baba atamtuma
kwenu kwa Jina Langu,
atawafundisha
mambo yote na kuwakumbusha
yote niliyowaambia.
“Huyo Msaidizi” maana yake ni wa karibu,
mwandani, kipenzi, mshirika au mbia. Kama ni mwandani wako ina maana
mnashirikiana katika kufanya “kitu/jambo”.
Rumi 8:9
Lakini ninyi,
hamtawaliwi na mwili, bali na
Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani
yenu.
Mtu ye yote ambaye hana Roho wa
Kristo, yeye si wa Kristo.
Rumi 8:14
Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu hao
ndio
watoto wa Mungu.
Kama Roho Mtakatifu anakaa ndani yako na
pia unaongozwa naye katika kila jambo, ile tu kuongozwa naye na wewe kukubali
kukuongozwa ina maana kuna tendo la ushirika kati yenu.Nachelea kuendelea mbele
zaidi juu ya Roho Mtakatifu maana ni somo pana litakuja kwa wakti wake. Ila
uelewe kuwa mwenye USHIRIKA na mwanadamu ni Roho mtakatifu.
Kwa hiyo kama Pendo ni Mungu, Ushirika
ni Roho Mtakatifu basi Neema iko kwa Yesu Kristo kama Paulo alivyowaandikia
makanisa mbalimbali. Naomba nikukumbushe kuwa somo letu ni juu ya Neema ya Yesu
Kristo.
NINI MAANA YA NENO NEEMA
Neno neema ni pana sana na linaweza kuchukuliwa
tafsiri kwa kulingana na tukio. Hizi ni baadhi tu ya maana ambazo tutaenda nazo
katika hili somo.
- · Ni kusaidiwa,kupewa msaada pale usipoweza au uliposhindwa ( helpful)
- · Ni kujali,kupewa uangalizi wa pekee, ( to care)
- · Kustahilishwa yaani unapewa stahili ambayo kihalali hukustahili/ hukutakiwa kupewa.
- · Kupendelewa, kupewa upendeleo katika jambo Fulani ambalo kwa utaratibu na uhalali hukustahili wewe kupata hilo jambao.
Yesu ndie ataoae neema kwa wanadamu. Tazama
maana ya “neema” kupitia mifano hii;
- i. Mungu pamoja na pendo lake huwa hachangamani na wenye dhambi (Yohana 9:31). Na kama hawezi (Mungu) kuchukuliana na mwenyedhambi nani wa kusimama kati ya mwanadamu mwenye dhambi na yeye? Maana mshahara wa dhambi ni mauti, ile tu kwamba umetenda dhambi basi, unastahili mauti ya vyote roho na mwili. Ndipo Yesu hutustahilisha mbele za Mungu kwa damu yake, anachosema mbele za Mungu kwa niaba yako ni kuwa “ ndio huyu Fulani kafanya dhambi hii na hii nah ii na anastahili kufa, LAKINI kumbuka nilikununulia na huyu Fulani kwa Damu yangu (Ufunuo 5:9), hivyo anastahili kupewa muda wa kutengeneza, usimue ( Luka 13:6-9). Hivyo pamoja na dhambi hufi ila umepewa upendeleo wa kuendelea kuishi wakati kiutaratibu wa Biblia usingepaswa kuendelea kuishi. Hii ndio Neema ya Yesu Kristo.
- ii. Wewe ambaye ni taifa nje ya Israel ( kimwili) haukupaswa kumkaribia Mungu, maana ulikuwa umelaaniwa kabisa, hukustahili hata kuliitia jina la Mungu wa Israel. Ndio maana biblia inakuita wa mataifa, yaani nje ya Israel. LAKINI baada ya kufa na kukufuka kwa Yesu Kristo akatuondolea laana tulioitwa wa mataifa akatuingiza katika zizi la Ibrahimu (Galatia 3:13-14, 29), kisha akatuistahilisha mbele za Mungu hata leo tunathubutu kuliitia jina la Mungu wa Israel, ooooooh haleluyaaaaa!! Sifa kwa Mwanakondoo aliyetununua kwa Damu yake.
- iii. Anapendelewa hata mbele ya mahakama ya mbinguni maana kwenye kitabu cha
Ufunuo 12:10-11
“Kisha
nikasikia sauti kuu mbingunii kisema,Sasa Wokovu na uweza na Ufalme wa Mungu
wetu umekuja na mamlaka yaKristo wake. Kwa
kuwa ametupwa chini mshtaki wa ndugu zetu,anayewashtaki mbele za Mungu usiku na
mchana.
11
-Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo na kwa neno la
ushuhuda wao. Wala wao hawakuyapenda ……”
- iv. Bila Jina Yesu usingestahili kuwa na Roho Mtakatifu ndani yako, na Roho Mtakatifu haji kwako tu sababu wewe umefanya kitu Fulani kizuri, bali Roho Mtakatifu huja mahali palipo na Jina la Yesu .
Yohana 14:26
“Lakini
huyo Msaidizi, yaani, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atamtuma kwenu kwa Jina Langu,atawafundisha mambo yote na
kuwakumbusha yote niliyowaambia”
Kwamba, yeye Yesu baada ya kufa ni yeye
aliyekuchagua wewe na akakupa Jina lake. Ile tu kukupa jina lake, Roho
Mtakatifu anakuja penye jina la Yesu. Mungu hamtumi Roho Mtakatifu kwakao
sababu umeokoka muda mrefu au sababu unatoa sadaka sana au sababu unapenda
kuomba. Mungu anatazama palipo na Jina la Yesu. Hivi ni baadhi tu ya mfano wa
namna ambavyo Yesu amejaa Neema kwako.
- v. Hii Neema ya Yesu inaenda mpaka kwenye maisha ya kila siku, kula kwako, kulala, kuamka, kuembea ni Neema ya Yesu. Hauna uwezo wowote juu ya hayo mambo ila ni Yesu tu ndio anakuwezesha.
Neema ya Yesu Kristo ndio inayokuunganisha na Pendo
la Mungu, ushirika wako na Roho Mtakatifu hata kukupa mahaitaji yako yote.
Unaishi sababu ya Neema yeke.
TUNAPATAJE NEEMA YA YESU KRISTO?
Kupitia hiyo mifano tumeona namna
ambavyo maisha yetu hayawezekani kuendelea mbele pasipo Neema ya Yesu Kristo. Swali
je Neema ya Yesu kristo inapatikana kwa kuiomba, kuifanyia tendo lipi hasa.
Ili mradi imeitwa Neema, ina maana
unapewa wakati hujakidhi matakwa na viwango vya kupata hicho kitu. Neema
hutolewa kwa matakwa (discretions) ya mtoaji. Huwezi wewe mpokeaji kwenda
kulazimisha au kuomba kuwa nipe jambo Fulani, na kama umepewa baada ya kuomba
hiyo si neema bali ni haki yako.
Haki ni kile kitu ambacho unapata sababu
tu aidha umekidhi masharti Fulani au kwa hadhi yako basi unastahili kupata hiyo
haki. Unapoomba kitu lazima uwe umejua kuwa umekidhi matakwa au kwa hadhi yako
unastahili kupata. Neema ni kinyume cha haki, kwakuwa hujakidhi matakwa na pia
hadhi yako haikuruhusu kupata lakini unapata.
Hebu tutazame mfano huu
- 1) wa Zaburi 23:1 inasema Bwana ndiye mchungaji wangu sitapungukiwa na kitu. Sasa mtu ambaye amekidhi viwango wa kuwa kondoo wa Bwana, huyu akipewa chochote au asipopungukiwa atakuwa amepewa haki yake, sababu amekidhi matakwa ya Kondoo. Yule ambaye hajakidhi matakwa yaani maisha yake ni ya ki mbuzi mbuzi na sio kondoo, pale ambapo atapewa kitu au hatapungukiwa kitu, huyu sio haki yake na hata alipoomba hakupewa sababu ya kuwa na haki, bali Huruma ( Neema) ya mtoaji ndio imempa hicho.
- 2) Wa mfungwa ambaye kafungwa gerezani kwa miaka kadhaa, ijapo sheria za nchi zinamruhusu raisi kuwatangazia msamaha wafungwa ambao wamekidhi viwango na masharti Fulani. Lakini ni matakwa ( discretion) ya raisi kumsamehe mfungwa Fulani na kumwacha mwingine ambaye makosa na miaka inafanana ya Yule aliyesamehewa. Huyu ambaye hajasamehewa hawezi kulalamika na kudai mahakamani kuwa na yeye afunguliwe. Pamoja na huyu aliyefunguliwa kupewa msamaha, hawezi kusema kuwa ilikuwa ni haki yake kuachwa huru eti kwa sababu amekidhi matakwa, swali litakuja na yule aliyeachwa ndani na wakati amekidhi matakwa?
Sasa hebu tuangalie biblia inasemaje juu
ya kupata Neema ya Yesu Kristo.
Ebrania 4:14,16
14
Kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu
kuliko wote ambaye ameingia mbinguni, Yesu Mwana
wa
Mungu, basi na tuyashike sana maungamo
yetu.
16
Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema na
kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.
Turejee mfano 2 hapo juu huyu
mfungwa anapoingia gerezani siku ya kwanza, anaanza kutumikia kifungo chake
akijua kuwa uhuru wake utapatikana muda wa kifungo ukiisha. Akiwa katika
mchakato wa kutumikia kifungo anaanza kutii mafunzo na masharti yote ya bwana
jela, anatii hayo si kwa sababu anataka kupewa uhuru mapema, bali ni kwa sababu
ya masharti ya kifungo chake. Akilini mwake anaendelea na maisha ya ufungwa
bila kutegemea kuwa kuna siku ataachiwa huru kabla ya muda kufika. Mtoa uhuru
wa huyu mfungwa anatazama maisha ya mfungwa ya kila siku, haya maisha ya kila
siku ndio humshawishi mtoa uhuru kuachia neema ya uhuru.
Sasa kutoka katika Ebrania 4,
tuliyoisoma inaonyesha kuwa kuna maisha Fulani ya mwanadamu ukiyaishi, na
katika mchakato wa kuishi hiyo namna ya maisha, basi Neema ya Kristo inakufikia
pasipo yeye kuitarajia. Waebrania anataja mfumo wa maisha ya namna hii-;
- KUSHIKA SANA MAUNGAMO.
Maungamo ni ukiri, yaani maneno
yatokayo katika kilindi cha moyo wako ambayo yamebeba uhalisia wa moyo wako.
Maana hakuna neno ambalo mwanadamu akatamka kama halijatoka katika kilindi cha
moyo wake. Biblia inasema kimjaacho mtu ndicho kimtokacho (Luka 6:45) na
aonavyo mtu ndani ya nafsi yake ndivo alivyo (Mith23:7). Kwa kila neno
unalolisema ujue ndivyo kulivyo ndani ya moyo na nafsi yako.
Ebrania anasema tuyashike maungamo
yetu, kuwa kusema kwa nje kunatokana na ndani kuko vipi, na unatakiwa kuchunga
sana ndani yako kuna nini. Kilichondani yako ndicho unachokikiri na kinatokea
kama unavyokikiri. Haijalishi mdomo utakuwa umeufunga au unatoa maneno, bali
ukiri utabaki palepale nafsi yako inaonaje hilo jambo.
Kwa kuwa ndani ya mtu(nafsi)
ndiko ukiri hutokea, basi inategemea hiyo nafsi imejaza nini. Kama imejaza
unyonge na kushindwa ujue ukiri wake utakuwa hivyo. Na kama nafsi imejaza
ushindi na Neno la kristo ujue ukiri utakuwa wa ushindi. Si unajua akuwa chanzo
cha imani ni kusikia, chanzo cha imani katika Kristo ni kusikaia Neno la Kristo
(Rumi 10:17). Nafsi inajazwa na kile ilichosikia, na ikishajaa ilichosikia
ndipo hapo nafsi huanza kutema/kukiri yaliyojaa ndani yake. Ukitaka kujua moyo
wa mtu umejaa nini sikiliza maneno yake, kama umejaa mpira wa miguu muda wote
hana mazangumzo mengine ni hayo tu, umejaa ushirikina muda wote atakuwa
anazungumza juu ya uchawi na waganga.
Kama amejaza Neno la Mungu hata
kama hajasema mstari wa biblia ila maneno yake yatakuwa ni ya hekima na Yesu
huwa na huyo mtu muda wote, maana Yesu ndio Neno lenyewe na pia Injili ya Yohana
inasema maneno yangu ( Yesu) yakikaa ndani yenu, Yeye Yesu na Baba watakaa
ndani ya huyo mtu . Kama Yesu, Baba na Roho Mtakatifu wanakaa ndani ya huyo mtu
ujue huyo mtu atakuwa anastahilishwa na kupendelewa katika maisha yake.
Imani chanzo chake ni kusikia
Neno la Kristo. Na imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo ni bayana ya
yale yasiyoonekana (Ebrania 11:1) maana yake
ukilipokea Neno ndani yako linakupa uhakika wa hilo jambo sawa na Mungu
aonavyo juu ya hilo jambo, hivyo ukiri wako unakuwa sawa na Neno na unakuwa ni
ukiri wenye kuumba vitu vyema na
vikatokea. Maana kwamba Neema ya Kristo inakuwa imetolewa (Neno),
ukilipokea Neno Yesu anakusaidia namna ya kulifanya hilo Neno liwe hai, ile
Yesu kukusaidia kulifanya Neno kuwa hai ndio Neema.
Kwa lugha rahisi ni kuwa Yesu
anaachilia Neema, Imani yako ndio mrija wa kupokea na kupitisha Neema. Mfano
kifo cha Yesu msalabani hii ni neema kwa Mataifa, na hii Neema ilikwisha
kutolewa kwa kila mtu, sasa mwenye Imani akilipokea Neno la msalaba ndani yake,
Yesu anamsaidia kulifanya hilo Neno kuwa hai, ndipo tunamwita huyo mtu
ameokoka.
Ebrania anatutaka tuwe makini na
ukiri wetu kwa maana huo ukiri ndio unaokusaidia kupata neema wakati wa
uhitaji. Yaani usipate shida wewe jaza Neno la Kristo ndani yako liishi hilo
Neno, ujue nyakati za uhitaji ukiri wako wa kila siku utakufanya upate
upendeleo na msaada ( neema) toka
kwa Yesu. Utakuwa sawa na mfano wa huyo mfungwa ambaye anaendelea kuishi kama
bwana jela atakavyo bila kujua na kujali kuwa kuna siku atatangaziwa uhuru kabla
ya muda. Usijaribu kuigiza katika ukiri wako, maana kikujazacho ndicho
kikutakacho, na ukijaribu kuigiza ukiri ili baadae uombe utakuwa sawa na yule
farisayo alikuwa anaomba kuwa yeye anafunga mara kadha kwa wiki na pia sio kama
Yule mtoza ushuru (Luka 18:9-14) sahau kupokea majibu ya maombi yako.
Kumbuka mwenye haki anaishi kwa
imani yake ( Ebrania 10:38) neema itakukuta njiani wakati unapoendelea kuishi
kwa Imani, na Neema inakuja kukusaidia pale usipostahili au usipoweza.
2.
KUKARIBIA KITI
CHA REHEMA
Kiti cha Rehema ni nini
Kutoka
25:17-22
17 nawe fanya kiti cha rehema cha dhahabu safi,
chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu naupana wa dhiraa moja na nusu.
22 nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti
cha Rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda,
katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israel.
Mungu
alimwelekeza Musa namna ya kujenga hema ya kukutania, katika vitu ambavyo
alimwelekeza weke ndani ya Patakaifu sana, kimoja wako ni kiti cha Rehema. Hiki
kiti kiliwekwa juu sanduku la agano, mstari
wa 22 unaeleza kusudi la kuwepo kwa kiti cha Rehema kuwa itakuwa ndio sehemu
ambayo Mungu ataonana na kuzungumza Musa mahali pale. Ina maana Musa alipotaka
kuzungumza na Mungu hakuenda tena mlimani kama hapo awali bali aliingia
patakatifu na kukaribi kiti cha Rehema.
Hayo
yalikuwa wakati wa agano la kale.Yesu alipokuja siku ya kufa kwake, pazia la
hekalu lilipasuka vipande viwili (Math 27:51) kumaanisha kuwa patakatifu sana
pa dunia hapatakuwa tena katika hekalu lililojengwa kwa matofali, nondo n.k.
maana Sanduku la agano lilitolewa duniani liko mbinguni (Ufunuo 11:19). Kila
mtu aliyempokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wake amepewa ujasiri wa kupaingia
patakatifu kwa kupitia Damu ya Yesu ( Ebrania 10:19-20).
Kiti
cha rehema hata sasa kipo na halisi huko mbinguni, soma
Ufunuo
8:3 inasema
3 Malaika mwingine aliyekuwa na chetezo cha dhahabu,
akaja na kusimama mbele ya madhabahu.Akapewa uvumba mwingi ili autie pamoja na maombi ya Watakatifu wote, juu ya
ile
madhabahu ya dhahabu iliyoko mbele ya
kile kiti cha enzi.
Kumbuka kazi ya Kiti cha Rehema cha
kipindi cha Musa ilikuwa ni Mungu apate kuona na kuzungumza na Musa hapo. Na
tafsiri rahisi ya maombi ni mazungumzo kati ya Mungu na mwanadamu. Ufunuo
anasema huyu malaika anayachukua maombi ya watakatifu kisha anayachanganya na
uvumba anafukisha juu ya kiti cha enzi.Maombi ya watakatifu huwa yanapokelewa
katika eneo liitwalo kiti cha Enzi. Mazungumzo ya Musa na Mungu ni kwenye kiti
cha rehema, na mazungumzo ya watakaifu na Mungu ni kwenye kiti cha Enzi.
Kiti cha rehema kilikuwa kwenye
madhabahu ya uvumba, na kiti cha Enzi kiko kwenye madhabahu ambayo pia kuna
uvumba.
Hivyo kiti cha rehema kipindi cha
agano la kale kilikuwa ni kivuli cha kiti cha enzi mbinguni.
Tukirudi kwenye Ebrania 4:16
anasema “…tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri ili tupewe rehema na kupata
neema ya kutusaidia..”
Ina maana Maombi, mazungumzo kati ya mwanadamu
na Mungu, ndio njia inayomfanya mwanadamu kukisogelea kiti cha enzi na hicho
kiti kimejaa neema ambayo huachilia rehema na hupelekea huyu mwanadamu kupata neema
ya kusaidiwa wakati wa uhitaji.
Haina maana kuwa ukiendee kiti
kwa ajili ya kuomba neema, ina maana unapokiendea kiti kwa ajili ya haki yako
au jambo lako lolote. Unapoendelea kuzungumza na Mungu juu ya hilo jambo, Yesu
anaachailia neema itakayokusaidia wakati wa uhitaji, hivyo wewe uliendea kiti
kwa jambo lingine ukitoka kwenye kiti unarudi na neema ya kusaidiwa nyakati za
uhitaji.
Kwa kadiri unavyokiendea kiti kwa
ajili ya mazungumzo na Mungu ndivyo unavyozidi kuongeza neema ya kukusaidia
wakati wa uhitaji.
Tazama Yesu alipowaambia
wanafunzi wake,kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni (Mathayo 26:41).
Hakumaanisha wakeshe na waombe wasiingie majaribuni, alikuwa anawahimiza kuwa
endeleeni kuzungumza na Mungu juu ya maisha yenu na mtakapokuwa mnaendelea
kuzungumza na Mungu, mtapokea neema ambayo hata jaribu kilikija halitakuwa
jaribu kwenu maana mna msaada wa ziada wa kuwafanya lisiwe jaribu kwenu
HITIMISHO
Usijaribu kuomba Yesu akupe
neema, Neema haiombwi anatolewa jinsi apendavyo yeye (Yesu). Wewe unapaswaa ubadili mfumo wa
maisha yako, uishi maisha ya Imani, yaani kulitii Neno na kuwa halisi kama Neno
liatakavyo. Ukiweka nia na kiu ya kuliishi Neno yeye Yesu ataachilia Neema yake
ya kulipata, kulielewa na kuliishi Neno. Kwa maana huwezi kuliishi Neno kwa
akili na nguvu zako.
Pia Maombi kwa uongozi wa Roho
Mtakatifu yawe ndio maisha yako ya kila siku, muda wowote na popote pale ulipo.
USHAURI
Kwa wewe ambae unasoma somo hili
na hujampa Yesu maisha yako awe Bwana na mwokozi wako, kumbuka Neema yake
imekwisha kutolewa ni wewe tu Kuamini na kukubali na kumruhusu Yesu aingie
ndani yako. Usiogope utaishi vipi maisha ya wokovu. Wewe amini kuwa alikuja
duniani na akafa kwa ajili yako,na kiri kwa kinywa chako kuwa umwenye dhambi na
unaomba toba ( geuka) na mruhusu atawale maisha yako. Yesu atachilia Neema
itakayokusaidia kukua katika wokovu.
Kama
uko tayari omba sala hii
“
Yesu mimi ni mwenye dhambi, nisamehe dhambi zangu. Nilikuwa mbali nawe narudi
kwako, nipokee kama mwana wako.nakubali kukupa moyo, nafsi na mwili wangu viwe
vyako kwa ajili yako. Amen
Kama umefanya sala hii kwa
kumaanisha, tayari umeokaka na Yesu yu pamoja nawe akusaidi.
Hongera kwa kuokoka.
Ni Mimi mwalimu wa injili
Mrs. Doris Barnabas Daniel

No comments:
Post a Comment